Mwaka huu umekuwa mzuri sana kwa mtu wetu Diamond Platnumz kwani amekuwa wa kupokea na kutajwa kwenye tuzo nyingi sana kwa mwaka huu wa 2015 na siku chache zilizopita Diamond Platumz alitajwa kuwania tuzo nyingine tena za kimatatifa MTV EMA 2015 jijini Milan Italy.

dai2
Headlines za Diamond Platnumz haziishii hapo, good news kwako mtu wangu msanii wetu wa Bongo Flava anazidi kuonyesha ubora wake kwenye nafasi mbalimbali za tuzo AfricaDiamond amepokea ushindi wa tuzo nyingine tena! African NAFCA Awards 2015 imemtaja Diamond kuwa Msanii wa mwaka anaependwa na wimbo wa Nana’ umetajwa kuwa Wimbo wa mwaka unaopendwa!
dai5
Kupita page yao ya Instagram @africannafca walipost picha hizi za tuzo za Diamond Platnumz
dai4
1.Diamond Platnumz favorite artist of the year.
dai3
2.Favorite Song of the Year – NANA wa Diamond Platnumz.
Na kupitia page yake ya Instagram, Diamond Platnumz amepost picha ya tuzo zake na ujumbe wa shukrani kwa mashabiki wake…
>>> “Hata nikisema niwashkuru, maneno hayataweza kuelezea Shukran zangu kwenu…. ila sikuzote ningependa mfahamu kuwa Nitaendelea kuhaso hadi jasho langu la Mwisho, kuhakikisha Mziki wetu una acha kudhalauliwa na Kuheshimiwa kama Miziki ya wengine… -Msanii wa Mwaka Anaependwa -Nyimbo ya Mwaka Inayopendwa #NANA 🙏 <<< @diamondplatnumz.

Hongera na Big Up sana Diamond Platnumz!

Post a Comment