Wakati baadhi ya vyama vya siasa vikionyesha kuwa na wasiwasi kufuatia kuondolewa ama kubadilishwa kazi kwa baadhi ya watendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi mwenyekiti wa tume hiyo jaji mstaafu Damiani Lubuva amevitaka kuacha kuingia utendaji wa tume hiyo kwani tume haiongozwi kwa maagizo ya wanasiasa.

Mwenyekiti huyo ameyasema hayo alipokutana na watu wanaoishi na ulemavu na kusema kuwa mabadiliko yanayofanyika ni ya kiutendaji tuu na wala hayana uhusiano wowote na jinsi ambavyo wanasiasa hao wanavyosema kuwa ni mbinu za kutaka kuiba kura.
 
Naye katibu mkuu wa shirikisho la watu wenye ulemavu kutoka Kilimanjaro Bw Kawawa Salim amesema watu wenye ulemavu wa kusikia wanashindwa kufuatilia mikutano ya kampeni kutokana na kukosekana  wakarimali na hivyo kushindwa kujua ahadi zinazotolewa na wagombea.
 
Awali akitoa mada katika mkutano huo kaimu mkurugenzi wa tume Bw Emanueli Kavishe amesema kwa sasa tume imejipanga vyema na hasa katika vitambulishio vya kupigia kura ambavyo ni vya kisasa na mtu hawezi kuvihujumu kiurahisi.
 

Post a Comment