Siku zote nitahakikisha nakusogezea kila stori inayonifikia na hapa stori ninayotaka kukupatia ni hii kutoka kwa mtayarishaji Sheddy Clever ambaye alizichukua headline hivi karibuni baada ya kutayarisha single mpya ya Diamond na staa kutoka Marekani Neyo.

Mtayarishaji huyo  alipokutana na ripota wa millardayo.com leo Sept 10 aliweza kuzungumzia collabo hiyo na jinsi Diamond alivyomfundisha Neyo maneno ya kiswahili katika single hiyo mpya.
.
.
Kwanza kabisa nimefurahi baada ya Diamond Platnumz kuniambia kuwa nahitaji kwenda Nairobi kwenda kutayarishaji single yake mpya aliyomshirikisha Neyo kwa kweli nashukuru sana uongozi mzima wa WCB wakina Babu Tale na Diamond kwani sikuwahi kuwaza kuja kufanya kazi na Neyo, miongoni mwa single zake ninazozikubali ni ule wa So Sick’ – Sheddy Clever
.
.
Siwezi kuzungumzia ni maadhi gani ya wimbo walioufanya ila watu wakae tu mkao wa kuupokea single hiyo mpya, kama vile watu mnavyojua Diamond amekuwa akijituma kwa hali na mali kuinua soko letu la Tanzania  hasa kwenye upande wetu wa muziki neyo kaimba Kishwahili katika single hiyo Diamond alimuimbisha Kiswahili siwezi kusema ni maneno gani ya kiswahili bali watu wakae mkao wa kula’ – Sheddy Clever

Post a Comment