Msafara wa mgombea wa nafasi ya urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, Mh.Edwrad Lowassa umejikuta ukizuiwa mara kwa mara na mamia ya wakazi wa wilaya za Korogwe na Handeni wakati alipokuwa akitoka Tanga kuelekea jijini Dar es Salaam.

Msafara huo wa mgombea wa nafasi ya urais Mh.Edwrad Lowassa haikuwa rahisi hata kidogo kufika mapema jijini Dar es Salaam akitoa jiji Tanga baada ya mamia ya wananchi kuvamia mara kwa mara msafara huo katika barabara kuu.
 
Lakini tukataka kujua dhamila kuu ya wananchi hawa kuvamia msafara wa mgombea huyo wa nafasi ya urais.

 Akiwa mjini Korogwe akalazimika kusitisha msafara wake na kuamua kuwaleza nini atalifanyia jiji la Tanga punde atakapochaguliwa.

Akatumia pia fursa hiyo kuutangaza mwezi januari 2016 kuwa mwezi wa neema kwa watanzania hasa wa kipato cha chini.
 
Msafara huo uliokuwa ukiongozwa na jeshi la polisi kutoka Tanga hadi Dar es Salaam ulisimamishwa mara kwa mara na wakazi wa maeneo ya Muheza, Korogwe, Michungwani, Kabuku, na Mkata ambapo walitumia fursa hiyo kumueleza changamoto zinazowakabili.
 
 Hatimaye Mh.Edward Lowassa na msafara wake wakalazimika kuzungumza na maelfu ya wakazi hao Muheza, Korogwe Michungwani, Kabuku, Mkata.
 

Post a Comment