Timbulo: Niliumizwa na usaliti wa Dr Slaa, kuliko Aunt Ezekiel na Ray Kigosi.

Timbulo ni moja kati ya wasanii walioonesha milengo yao kisiasa mwaka huu, Hit maker huyu wa ‘Domo langu’ ameonekana kwenye ‘stage’ za UKAWA mara kadhaa.


Akizungumza kupitia kipindi cha The jump off cha Times FM, timbulo ameelezea mtazamo wake kuhusiana na kitendo cha  wasanii wa filamu Aunt Ezekiel na Vicent ‘Ray’ Kigosi kuhama UKAWA walikokuwa wakishabikia mwanzoni kwenda Chama cha mapinduzi CCM.
Mkali huyo amesema haikumshitua sana, kwa kuwa matukio kama haya yamekuwa yakijitokeza mara kadhaa.

“kila mtu ana maamuzi yake, wao wamefanya wanachoona kina manufaa kwao, ila wananchi wanataka mabadiliko, amesaliti Slaa, Lipumba sembuse wao? haijaniumiza hata kidogo, aliyeniumiza ni Slaa niliyepoteza kura yangu 2010 kwa ajili yake” alisema Timbulo.

Post a Comment