pricing
Najua nina watu wangu wanataka kufahamu ni nchi ipi inayoongoza kwa Uchumi barani Afrika, sasa basi leo nimekusogezea  nchi 5 zinazoongoza kwa Uchumi barani Afrika;
Nafasi ya tano (5)  imetajwa ni Morocco

.
.
Wanasema Uchumi wa Morocco unategemea zaidi Utalii, sekta ya Mawasiliano, viwanda vya nguo,Kilimo pamoja na miji ya marrakech na Rabat ni moja ya miji inayopokea idadi kubwa ya watalii duniani.

Nafasi ya nne (4) imetajwa ni Algeria
.
.
Algeria imeshika nafasi ya nne katika nchi ambazo zinaoongoza kwa kuwa na uchumi mkubwa wa Afrika taifa la kaskazini mwa Afrika imeingia katika orodha hiyo.Na moja kati ya sekta inayoiletea uchumi ni usafirishaji wa Mafuta.
Nafasi ya tatu (3) imetajwa ni Nigeria
.
.
Wataalamu wa mambo wanasema  Mwaka jana Nigeria ilishika nafasi ya kwanza lakini uchumi wake umeshuka kwa kipindi hicho ambapo  utawala wa rais wa zamani Goodluck Jonathan ulikuwa ukimaliza muda wake.Nigeria inategemea sana Mafuta ambayo yanapatikana kwenye taifa hilo, ukiondoka mafuta pia Nigeria katika sekta ya Mawasiliano na teknolojia , Burudani hasa muziki na Filamu zimekuwa na mchango mkubwa sana katika taifa hilo.

Nafasi ya pili (2) imetajwa ni Misri
.
.
Misri imetajwa kushika nafasi ya pili kati ya mataifa matano yenye uchumi mkubwa Afrika na kama isingekuwa matatizo ya siasa ambayo yametetemesha hali ya amani kwenye taifa hilo basi huenda ingekuwa ya kwanza.Misri ni moja kati ya mataifa ya kwanza katika ulimwengu huu na kubuni teknolojia kadhaa ikiwemo, Kilimo, Hesabu, na Ujenzi.

Nafasi ya kwanza(1) imetajwa ni South Africa
.
.
Nigeria ndio ilikuwa imeshika nafasi ya kwanza katika nchi  zinazoongoza kwa uchumi barani Afrika lakini kwa sasa ni Afrika Kusini chanzo kikubwa cha ubora wake  kwenye uchumi ni biashara ya madini na Utalii.

Post a Comment