Utafiti uliofanywa na taasisi inayojisughulisha na masuala ya kitafiti ya Twaweza umebainisha kuwa chama cha mapinduzi CCM ndio chama kinachaopendwa zaidi na wananchi kwa asilimia 62.


Akiwasilisha matokeo ya utafiti huo mkurugenzi wa Twaweza Bw Aidan Eyakuze amesema chama cha demokrasia na maendeleo Chadema ndio chama kinachoshika namba ya pili kwa kupendwa na watu ingawa utafiti pia umeonyesha kuwa idadi ya watu wanaosema kwamba watawachagua wagombea wa Chadema katika ngazi ya urais, ubunge na udiwani imepungua kidogo.
 
Aliyewahi kuwa mjumbe wa bunge maalum la katiba Bi Maria Sarungi akitoa maoani yake kuhusu utafiti huo amesema hayo ni matokeo tuu na wala siyo lazima siku ya mwisho ya kupiga kura hali ibaki kuwa vilevile bali jambo la msingi ni vyama vya upinzani kuongeza nguvu katika kujitambulisha kwa umma.
 
Naye mwenyekiti wa kigoda cha Mwalimu Nyerere Prof Penina Mlama  amesema utafiti huo ni mapema sana kwa sasa kukubali ama kuukataa kwani kuna vitu vingi vya kuangalia kama vilizingatiwa katika utafiti huo ambapo Bw Stepheni Robert mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuo kikuu cha Dar es Salaam anayechukua masula ya sheria amesema utafiti huo unamapungufu chungu mzima ikiwemo kitendo cha kuwapa simu wale wanaohojiwa alafu utegemee majibu tofauti.
 

Post a Comment