Mgombea ubunge kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) jimbo la kahma mjini James Lembel katika mikutano yake ya kampeni iliofanyika katika kata za Mwendakulima na Nyasubi wilayani humo.

Lembeli amesema kiongozi bora ni Yule anayetekeleza maendeleo na sio kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki.
Amesema endapo wananchi watachagua chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA, watahakikisha serikali hiyo inatatua matatizo ya wananchi kwa kuwekeza katika elimu na upatikanaji wa huduma za afya.

Amesema elimu ndio urithi pekee kwa mtoto, hivyo Chadema imejipanga kuhakikisha inatoa elimu bure ili kuwasaidia watanzania kuondokana na umasikini unaochangiwa na kukosa elimu.

Akiwa katika kijiji cha Busalala kata ya Mwendakulima, Lembeli amewapongeza wananchi kwa kushirikiana nae katika uongozi wake uliopita, katika ujenzi wa shule ya msingi Busalala iliyopo katani humo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CHADEMA wilayani humo Juma Protas amewataka wananchi kupuuza wanasiasa wanaowapotosha wananchi kwa kuwapa pesa na vitu vidogovidogo ili wasiende kupiga kura.

 

Protas amesema vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za msingi na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano mara wanasiasa hao wanapojitokeza ili kuwabaini na kuchukuliwa hatua.

Post a Comment