Aliyekuwa rais wa Guatemala Perez Molina ambaye alijiuzulu jana ameonja machungu ya mahabusu baada ya kulala humo usiku wa kuamkia leo kabla ya kupandishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.


Molina amelala mahabusu ikiwa ni utekelezaji wa amri ya mmoja kati ya majaji wa katika mahakama ya nchi hiyo ambaye aliamrisha akamatwe na kuwekwa chini ya ulinzi wa vyombo vinavyosimamia wahalifu nchini humo huku taratibu za kumfikisha mahakamani kukabilina na mashtaka ya ubadhirifu zikamilishwa.
 
Majira ya asubuhi Molina alifikishwa mahakamani huku akizongwa na camera za waandishi wa habari na kisha kupanda kizimbani kukabiliana na mashtaka ambayo yanamkabili ya kulisababisha hasara taifa hilo na kupokea rushwa vitu ambavyo ni kinyume na katiba ya Guetemala.
 
Katika mashataka hayo mahakamani hapo Perez Molina alidaiwa kupokea rushwa ya dola za marekani milioni tatu nukta saba kutoka kwa wafanyabiashara nchini humo ili aweze kutoa maagizo kwa serikali yake, maagizo ambayo yatawasaidia wafanyabiashara hao.
 
Molina amefikishwa mahakamani baada ya maandamano ya muda mrefu ya kumpinga kutokana na kudaiwa kupokea rushwa huko ambapo baada ya maandamano hayo bunge la nchi hiyo lilimuondolea kinga ya kutoshtakiwa na saa chache baadaye yeye kujiuzulu na kisha kukamatwa na kushtakiwa.
 

Post a Comment