Prof. Lipumba akana kutumika na CCM

Aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF – Prof. Ibrahimu Lipumba amekana tuhuma anazodaiwa kutumika na chama tawala cha CCM kuuvuruga umoja wa wapinzani nchini.


Wakati akihojiwa na Azam Tv kwenye taarifa ya habari hapo jana jioni, Mwandishi alimtaka Lipumba ajibu tuhuma hizo za kutumika na chama cha Mapinduzi CCM ili kuharibu nguvu kubwa iliyopo sasa kwa vyama vya upinzani vinavyounda Katiba ya Wananchi – UKAWA.

“Sisi ndio wapinzani wakweli, mimi nilijiunga na CUF mwaka 1999, na tangu hapo ndio nilikuwa mpinzani mkuu wa CCM, iweje sasa nitumike na CCM kuua Upinzani?, situmiki na CCM “, alijibu Lipumba.

Lipumba pia amekana taarifa zilizozagaa siku ya jana kuwa alikuwa anataka kuongea na waandishi wa habari, na kusema kwamba habari hizo zilikuwa ni uzushi mtupu.
Source – Azam TV

Post a Comment