Licha ya serikali kufunga migodi 5 yenye migogoro ya mitobozano katika mgodi wa Tanzanite wa Milerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, uongozi wa chama cha ushirika wa wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite umepata wakati mgumu wa kuzima jaribio la genge la wachimbaji wadogo zaidi ya 200 maarufu kama wanaapolo kutaka kuvamia mgodi wa madini wa Tanzanite one unaomilikiwa na wawekezaji wa ndani wakipinga mwekezaji huyo kuwateka baadhi ya wachimbaji wenzao ndani ya mgodi huo kwa lengo la kupora madini.


Wakizungumzia tukio hilo lililotokea katika eneo la kitalu “B” wachimbaji hao wamesema mwekezaji huyo alitumia mwanya huo kwa askari wake kuvamia mgodi usiokuwa na mtobozano mali ya  Bw Saidi Nasoro Mwarabu mara baada ya kiberenge chake kuharibika na wakati walipokuwa kwenye matengenezo waligundua moshi uliokuwa ukitoka ndani ya mgodi huo na walipofuatilia ndipo walipokutana na moshi unaodhaniwa kuwa umesababishwa na mabomu ya askari wa mwekezaji huyo wakati wakitekeleza azma hiyo, na hali ilikuwa hivi.
 
Hata hivyo baada ya kukubaliana na ushauri wa mwenyekiti wa ushirika huo, ndipo walipoeleza kushangazwa na hatua ya mwekezaji huyo kutumia mwanya huo, hasa baada ya kuona mgodi huo ndio unaonyesha neema ya kupatikana kwa madini ya Tanzanite wakilalamikia askari hao kukiuka sheria, kanuni na utaratibu wa kuingia na silaha ndani ya mgodi.
 
Hata hivyo licha ya jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi zikiendelea, meneja mahusiano wa kampuni hiyo ya Tanzanite One Bw Khalfani Mbezi alipoulizwa juu ya vurugu hizo amesema wachimbaji hao wamekuwa wakikiuka sheria kwa kuvuka mipaka na kuingia ndani ya eneo la Tanzanite One.
 

Post a Comment