Mwanasheria wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu, amesema tuhuma zilizotolewa na aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho Dr Wilibrod Slaa, si za kweli na anaongozwa na tamaa za madaraka.

Akizungumza jana jioni na redio idhaa ya kiswahili ya DW, Tundu amedai Dr Slaa ndio alihusika kufanya mpango wa kumkaribisha mgombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa CHADEMA na si vinginevyo.

“Mshenga ni Gwajima hajajisema yeye mposaji, kilichoharibika ni First Lady mama alikataa siku ambayo kamati kuu ilimpokea Lowassa Dr alilala nje alitupiwa mabegi yake akalala kwenye gari kesho yake akasema hataki anataka kujiuzulu.

kama nmemsikia sawa sawa amesema yeye hana chama, juzi amepokea mshahara wa chama, nyumba anayokaa imenunuliwa na chama walinzi alionao ni wa chama, anatukana chama wakati bado amechukua mshahara wa ukatibu mkuu wa chama juzi”

Katika ‘line’ nyingine, Lissu ameongeza kuwa Lowassa alihojiwa na kamati kuu kuhusu kashfa za ufisadi wa Richmond, na kudai aliyefanikisha mkataba kusainiwa ni Rais Kikwete si yeye (Lowassa).

Post a Comment