Tume ya uchaguzi ya Zanzibar imewapitisha wagombea kutoka vyama 14 kugombea urais wa Zanzibar katika uchagzui mkuu mwezi wa Oktoba mwaka huu.


Akitangaza uamuzi huo wa tume mkurugenzi wa tume ya uchaguzi Salum Kassim Ali amesema tume imeridhika na wagombea hao wakiwemo CCM, CUF na TADEA na sasa na majina hayo yatabandikwa nje kwa masaa 24 ili kama kutakuwa na pingamizi  watapitia na kutolea maamuzi ndani ya masaa 24.
 
Mapema wagombea wa vyama 10 kati ya 11 waliobaki walikamilisha utaratibu wa tume ya kuwasilisha fomu na ada ya shilingi milioni mbili   huku mgombea wa mwisho wa chama cha NRA Seif Ali Iddi aliwasilisha fomu zake kukiwa kumesalia dakika 3 bada ya kupata ajali akiwa njiani kuja ofisi za tume, hata hivyo alifanikiwa na tume kumpokea na jina lake kubandikiwa kuwa mgombea urais wa Zanzibar.
 
Wagombea wengine waliofika wakati wa asubui katika ofisi za tume ni pamoja na mgombea wa chama cha Jahazi asilia Kassim Bakari Ali ambaye alifika akiwa katika gari maalum na baadaye akafuata mgombea  wa ADC Bw Hamad Rashid akiwa ameonganzana na wafuasi wa chama hicho ambapo wagombea wote hao walilia haki  na huru katika uchaguzi mkuu.
 
Kampeni za urais wa Zanzibar zinatarajiwa kuanza rasmi kuanzia  jumatatu jioni huku kukiwa hakuna dalili ya kuwepo pingamizi kutoka kwa mgombea yeyote, zoei hilo limeshudia wagombea 15 wakijitokeza kuwania urais wa Zanzibar mwaka huu tafauti na uchagzui ulipita walikuwa wagombea saba, chama pekee amabcho  
kimeshindwa kurejesha foumu ni cha updp ambaye mgombea wake alikuwa mwanmke  mwajuma ali khamis.

Post a Comment