Watu watatu wamekufa na wengine thelathini wamelazwa hospitalini kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu nchini Tanzania na hasa katika mji wa kibiashara wa Dar es salaam.
Wataalamu wa afya wamesema kwamba mlipuko huo unapatikana kwenye maeneo ambayo hayana usafi wa kutosha na vyoo vya kisasa hasa katika maeneo yenye msongamano wa makazi katika jiji hilo.
 
Maafisa wa afya tayari wameshachukua hatua ili kuzuia mlipuko huo usienee zaidi tangu mlipuko mkubwa wa kwanza ulioripotiwa kulikumba jiji hilo mwaka 2009.
Wodi tengefu kwa wagonjwa wa ugonjwa huo imeshaandaliwa katika hospitali za wilaya ya Kinondoni eneo ambalo limeathiriwa vibaya na ugonjwa huo.




Umma wa watanzania wametakiwa kuwa waangalifu baada ya kifo cha mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka ishirini na saba,mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuonesha dalili zinazoshabihiana na magonjwa ya milipuko.
Dar es salaam ni mmoja kati ya miji yenye idadi kubwa ya watu, mji huo pekee una idadi ya watu zaidi ya milioni tano.
Watu waishio katika makazi holela wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa ugonjwa wa kipindupindu kutokana na kutokuwa na vyoo bora na vya kisasa .


Post a Comment