Muda mfupi kabla mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga Bw.Fred Mpendazoe kurudisha fomu baadhi ya wanachama wa chama hicho wameandamana na kuvamia ofisi ya chama kwa madai kuwa hawakubaliani na kitendo cha kamati kuu ya wilaya kubadilisha matokeo ya kura za maoni na kumtangaza mgombea wasiyemtaka kugombea nafasi hiyo.

Wakizungumza na ITV baadhi ya wanachama hao wamedai kutokubaliana na mapendekezo ya kamati kuu kubadilisha jina la mgombea wao Bw.Donald Kahema waliyekuwa wamemchagua kwa kura mia mbili tisini dhidi ya Fred Mpendazoe aliyepata kura kumi na moja hali inayoonyesha baadhi ya viongozi wanakitumia chama vibaya kwa maslahi binafsi na kutishia kuvuruga chama ambacho wananchi walikiamini kwa muda mrefu kuwa kinaweza kuleta mabadiliko ya kidemokrasia.
 
Aidha katibu muenezi chadema wilaya ya kishapu Bw.Martin Ganja amekiri kuwepo kwa hali hiyo huku akidai kuwa kamati kuu imekiuka na kupora haki za msingi za wapiga kura na yeye kama kiongozi atasimama imara na kuhakikisha kuwa anapigania haki na maslahi ya wanachama.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa chadema wilaya ya kishapu Bw.Paulo Magembe amesema kimsingi wanachama wana haki ya kudai haki zao huku akidai kuwa kamati kuu ina wajibu wa kuona ninini wanachama wake wanahitaji ili kukiepusha chama kuingia katika migogoro inaoweza kusababisha chama kuanguka katika uchaguzi mkuu ujao.
 
source by ITV

Post a Comment