Mgombea urais wa chadema kupitia (UKAWA)Mh.Edward Lowasa ametembelea baadhi ya vituo vya mabasi yanayotoa huduma katika jiji la Dar es Salam na vyenye kero kubwa kikiwemo cha gongo la mboto kwa lengo la kujionea adha ya usafiri    wanayopata wananchi ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kuondoa kero hiyo kama  wananchi wakimchagua kuwa rais wa awamu ya Tano

Mhlowasa aliyeambatana na mgombea mwenza Mh.Duni Haji baada ya kufika katika  kituo hicho hakuishia tu kuwatazama wananchi wanavyotaabika na usafiri bali  aliungana nao kusafiri kwa kutumia moja ya dala dala inayotoka Gongo la Mboto  kwenda Kisarawe na kushuka chamazi na kisha akatumia usafiri wa gari ndogo za  abiria aina ya Noah kutoka chamazi hadi Mbagala.
 
Licha ya kuwa ziara hiyo ilikuwa ni ya kustukiza ilivuta umati mkubwa wa watu  wa rika mbali mbali wengi wakiwa vijana ambao waliacha shughuli zao na kuanza  kuwafuata viongozi hao wakitaka kusikia walau sauti zao na licha ya mgombea  mwenza Mh.Duni Haji kuwatuliza kwa kuwaeleza kuwa watazungumza nao baada ya  uzinduzi wa kampeni waliendelea kuwafuata viongozi hao.
 
Wananchi waliokuwa kwenye maeneo hayo wamesema hatua ya viongozi hao wa ukawa  ya kufika kujionea wao wenyewe taabu na shida zinazowakabili licha ya kuwapa  matumaini ya kuondokana na tatizo hilo inadhihirisha adhima ya umoja wa ukawa  ya kuleta mabadiliko yaliyoshindikana kwa zaidi ya miaka hamsini.

Post a Comment