LAS VEGAS, NV - MAY 17: Singer Chris Brown and daughter Royalty arrive at the 2015 Billboard Music Awards at MGM Garden Arena on May 17, 2015 in Las Vegas, Nevada. (Photo by Gregg DeGuire/WireImage)
Msanii wa R&B Marekani Chris Brown siku hizi amekuwa mtu wa kuspend muda mwingi sana na mtoto wake wa kike, kila atakapo kwenda basi na mtoto Royalty yupo nyuma, sio siri mtu wangu ni wazi kuwa Chris Brown anaenjoy sana kuwa na kuitwa baba.
royalty3
Headlines za Chris Brown time hii kwenye kurasa za burudani ni ujio wa album yake mpya ambayo anategemea kuidondosha very soon, kizuri zaidi kuhusu album hii mpya ni jina aliloipa album hiyo!
royalty2
Royalty Brown mtoto wa R&B Superstaa Chris Brown
Chris Brown kaamua safari hii awape mashabiki wake kitu tofauti, kitu kitakachowagusa mioyo ya mashabiki kama vile ambayo mtoto wake kaugusa moyo na maisha yake… kupitia Twitter page yake Chris alichukua time na kuandika maneno machache yaliosema; “Album yangu mpya itaitwa ‘ROYALTY'”.
royalty
Tarehe ya uzinduzi wa album hiyo bado haijafahamika ila kwenye interview moja aliofanya Chris Brown na mtangazaji maarufu wa Radio Ryan Seacrest, Chris alisema hii ni kama zawadi kwa mtoto Royalty ambaye kayabadilisha maisha yake, na aliye mfanya atake kuwa baba bora na mwanaume bora.
royalty2
Kwa sasa Chris ametoka kutengeneza video ya wimbo wake Liquor siku chache zilizopita na very soon itasogezwa kwetu mtu wangu.

Post a Comment