Umeme wa kutumia gesi asilia unatarajiwa kuanza kutumika mwezi ujao ambao utaunganishwa kwenye Gredi ya taifa ilyopo kinyerezi jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari injinia Leonce Mroso kutoka kituo cha kuchakata gesi cha madimba kilicho mkoani Mtwara amesema wamefanikiwa kuifungua gesi kutoka kwenye visima na kusafirishwa kwenye kituo hicho kwa ajili ya kuchakatwa.
 
Amebainisha kuwa gesi hiyo  kwa sasa imechakatwa na inatarajiwa kusafirishwa kwenda Dar es Salaam eneo la kinyerezi  ili kuunganishwa kwenye Gridi ya taifa ifikapo tarehe kumi ya mwezi wa tisa ili iweze kuzalisha umeme.
 
Hata hivyo amesema gesi hiyo inafaa kutumika majumbani na tayari utafiti umefanyika katika baadhi ya mikoa ikiwemo mkoa wa Dar es Salaam, Mtwara na Lindi.
 
Kituo hicho kinauwezo wa kuchakata gesi futi za ujazo milioni 80 kwa siku lakini lengo ni kuchakata futi za uchazo milioni miambili na 10 kwa siku.

Post a Comment