Vyama vilivyoshindwa kukidhi vigezo ni CCK, TADEA, DP na AFP amabyo imeingia mitini ambapo akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi za tume baada ya tume kuwatangazia kushindwa kukidhi vigezo mwenyekiti wa CCK Bw Costantine Akitanda amesema.

Wagombea urais waliowahi mapema asubuhi ni Mh Edward Lowassa Chadema na Dk Jonh Magufuli wa CCM ambapo kwa nyakati tofauti waliowasili ofisi hizo za tume wakiwa na wapambe wao wachache na mara baada ya kuidhinishwa na mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi wakapata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari.
 
Wagombea wengine waliofika majira ya mchana ni mgombea urais kupitia TLP Maxmilian Lyimo na mgombea urais kupitia ACT Bi Anna Mghwira ambaye ni mwanamke pekee aliyeingia katika kinyang'anyiro hicho kwa uchaguzi wa mwaka huu ambaye chama chake kimemteua siku chache kabla ya ukomo wa kurudisha fomu lakini pia kimevunja rekodi kwa kutafuta wadhamini kwa siku moja na hatimaye kukidhi vigezo vya tume.
 
Katika zoezi hilo vituko vya hapa na pale navyo havikukosekana katika ofisi za tume ya uchaguzi baada ya mgombea urais kupitia tiketi ya chauma kufika katika ofisi hizo na kujikuta akiwa hana picha hivyo kulazimika kurudi nyumbani kuzifuata huku akirudi dakika za majeruhi lakini pia wapo walioelezea changamoto walizokumbana nazo wakati wa kutafuta wadhamini.
 
Mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi jaji Damian Lubuva akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukamilisha zoezi hilo ametolea ufafanuzi baadhi ya mambo ikiwa ni pamoja na walioshindwa kukidhi vigezo huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi katika eneo hilo la tume ya uchaguzi.

Post a Comment