Mgombea Ubunge katika Jimbo la Ludewa kwa tiketi ya CCM Bw. Deo Filikunjombe, amepita bila kupingwa wilayani humo baada ya Mgombea wa Chadema kushindwa kutimiza Masharti na Taratibu za Ujazaji wa Fomu.

Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya ya Ludewa, Ndg. Wiliam Waziri amesema leo kuwa Mgombea wa Chadema ameshindwa kutimiza taratibu za ujazaji wa fomu hizo hivyo kukosa sifa ya kuwa Mgombea wa Ubunge.

Ndg. Waziri amesema kwamba Kati ya wagombea wanne waliochukua fomu aliyetimiza taratibu ni Mgombea wa CCM, Bw. Deo Filikunjombe pekee;

Wagombea wa DP na TLP waliishindwa kabisa kurejesha fomu huku Mgombea wa Chadema akishindwa kujaza fomu vizuri na kushindwa kurejesha Fomu ya Kiapo cha Maadili ya Sheria za Uchaguzi.

Post a Comment