Mgombea urais kwa tiketi ya chama cha mapinduzi Dr John Pombe Magufuli ameonesha kushangazwa na miradi kadhaa ya maendeleo nchini kukwama katika sekta mbalimbali huku fedha zikiwa zimeshatolewa jambo linalowafanya watanzania kuichukia serikali yao na kusababisha mianya ya rushwa na hivyo kuwataka watanzania wampe ridhaa ya kuliongoza taifa ili aweze kuisimamia miradi hiyo kikamilifu na kuleta maendeleo nchini lakini pia kubana fursa za ubadhirifu zinazosababisha kero kubwa kwa wananchi wa hali ya nchini.

Akitokea mkoani Rukwa kuelekea mkoani Mbeya mgombea huyo wa kiti cha urais kupitia chama cha mapinduzi Dr John Pombe Magufulia ambaye ameonekana kuungwa mkono na makundi mbalimbali wakiwemo walemavu na viongozi wa dini mbalimbali hapa nchini amezungumza na maelfu ya wakazi wa Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia amewaambia watanzania kupitia wakazi hao kuwa katika utendaji wake wa miaka 20 serikalini hakuwai kuonywa ama kufukuzwa na ametekeleza majukumu yake kwa weledi na uadilifu mkubwa kutokana na kiu yake ya kutaka kuona watanzania wanapata maendeleo ya kweli hasa wale wananchi wa kipato cha chini.
 
Aidha Dr Magufuli amesema endpo atapata ridhaa ya watanzania kuliongoza taifa wananchi watashangazwa na namna nchi itakavyopiga hatua mbele za kimaendeleo kwa kuwabana wale wote wanaopaswa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kuwa nao maeneo ya kazi jambo litakalosaidia kuzuia pia ubadhirifu.
Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi Mh William Lukuvi amemfananisha Dr Magufuli kama tingatinga lenye uwezo wa kung’oa magugu yote katika sekta mbalimbali kiwemo kero za rushwa, ubadhirifu na urasimu unaofanya maendeleo kurudi nyuma.
 
Dr Magufuli anatarajiwa kuendelea na ziara yake mkoani Mbeya baada ya kuzungumza na wakazi wa maeneo mbalimbali ikiwemo Tunduma ambapo mamia ya wakazi wa maeneo hayo walijitokeza kumlaki na kumsikiliza ambapo imeelezwa amevunja historia ya mikutano mikubwa iliyowahi kufanyika katika maeneo hayo.
 


Post a Comment