Watanzania wametakiwa kuwa makini hasa wanapotumia mitandao ya kijamii kwani serikali imejizatiti kuhakikisha sheria zote mbili za mitandao na ile ya miamala inatekelezwa kwa kwa mujibu wa sheria.
Licha ya sheria hizo mbili zilizopitishwa na bunge mapema april mosi huku zikitajwa kuwa ni tata na kandamizi kwa watumiaji wa mitandao , serikali inasema sasa ni rasm utekelezaji wake sept mosi mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa sheria hiyo ya mitandao ya mwaka 2015, inatoa nafasi finyu kwa mtumiaji wa mitandao huku ikipiga marufuku, kutuma jumbe zisizo thibitishwa, picha za utupu, jumbe zozote zenye lengo la kudhalilisha ikiwa ni pamoja na taarifa zenye lengo la kuposha umma, watumaji wanasema wamejipanga kutekeleza.
 
Lakini kwa mujibu wa mtaalam wa masuala ya ICT kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam Bw Moses Ismail anasema licha ya sheria hiyo kali ni dhahili serikali italazimika kutumia nguvu kubwa kwani teknolojia haina mipaka.
 
Sheria hizo mbili zilizopitishwa bila baraka za kambi rasm ya upinzani bungeni, serikali inasema Tanzania si nchi ya kwanza kuwa na sheria kama hizi, kwani pamoja na mambo mengi itasaidia kupunguza nyingi zinazotokana na matumizi hasi ya teknolojia.
 
Wakati utekelezaji wa sheria hizo ukianza mapema septemba mosi, baadhi ya taasisi za kisheria nchini ziko mafichoni sasa zikijipanga kuzipinga sheria hizo mbili mahakamani kwa madai si rafiki kwa watumiaji wa mitandao.

Post a Comment