KOCHA wa timu ya SIMBA B, NICO NYAGAWA amesema, kikosi chake kinaendelea vyema na mazoezi ya kujiandaa na mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya AZAM B
Timu ya SIMBA B
KOCHA wa timu ya SIMBA B, NICO NYAGAWA amesema, kikosi chake kinaendelea vyema na mazoezi ya  kujiandaa na mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya AZAM B, iliyopangwa kufanyika siku ya SIMBA DAY, AGOSTI NANE.
NYAGAWA, amesema, wanafanya mchujo wa mwisho ili kupata wachezaji 20 kutoka kwenye kikosi cha wachezaji HAMSINI wanaoshiriki mazoezi hayo ili wacheze kwenye mechi ya SIMBA DAY.
Wakati vijana wa SIMBA B,wanajifua jijini, DSM, kujiandaa na mchezo dhidi ya AZAM B, kaka zao wamepiga kambi ZANZIBAR wakijiandaa na mechi dhidi ya AFC LAOPARDS ya KENYA itakayochezwa siku ya SIMBA na ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara itakayoanza septemba 15

Post a Comment