Winga wa KIAGENTINA Angel Di Maria amejiunga rasmi na timu ya PSG ya UFARANSA toka timu ya MANCHERSTER UNITED kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 44
Winga wa KIAGENTINA Angel Di Maria
Winga wa KIAGENTINA Angel Di Maria amejiunga rasmi na timu ya PSG ya UFARANSA toka timu ya MANCHERSTER UNITED kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 44.
Baada ya kufuzu vipimo vya afya Vilivyofanyika  nchini QATAR, MUAGENTINA huyo amesema amefurahi mno kujiunga na timu hiyo na sasa amejipanga kupambana ili kuipa mafanio timu hiyo yenye nyota lukuki hasa kwenye michuano ya UEFA.
Ndani ya misimu miwili timu hiyo ya PSG imekuwa ikiishia kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya na Di MARIA amesema atajitahidi kwa uwezo wake wote japo aifikishe kwenye hatua ya fainali na kuchukua ubingwa.
Ikumbukwe kuwa Angel Di Maria mwaka jana alijiunga na MANCHESTER UNITED kwa ada ya uhamisho ambayo ilivunja rekodi kwenye soka la ENGLAND ya paundi milioni 59 ila baada ya msimu mmoja tu wa kuichezea timu hiyo ya OLD TRAFFORD ameihama tena baada ya kutokuwa na msimu mzuri.

Post a Comment