Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi taifa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete amesema mchakato wa uteuzi wa mgombea wa nafasi ya urais wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli umedhihirisha kuwa chama hicho hakiteuwi kada ama mwanachama yeyote kutokana na fedha zake na kwamba uteuzi wake umetokana na mapenzi ya mungu kwa Tanzania kumpata mtu atakayesimamia kwa dhati rasilimali za taifa na kuwatumikia wanyonge na asiyeyumbishwa na rushwa.

Akizungumza na wanaccm mkoa wa Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi taifa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete amewahakkishia wanaccm wote nchini kuwa chama hicho kina mgombea mzuri tena mzuri sana katika kila hali iwe na ya ucha mungu, uwajibikaji na uchapakazi kwa kuzingatia misingi ya haki na hana kigugumizi katika utendaji wake na kwamba ni mpango wa mungu Tanzania kumpata kiongozi mwadilifu atakayesimamia uwajibikaji na uadilifu na kwamba ni mtu asiyejikweza na kwamba ni mgombea wa sampuli nyingine.
 
Akielezea sifa za Dr John Pombe Magufuli mwenyekiti huyo wa CCM taifa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete amesema Dr Magufuli anachukia sana uzembe, rushwa na ubabaishaji lakini pia usawa wa kijinsia na ndo maana akamteuwa mgombea mweza kuwa mwanamke.
 
Mgombea wa kiti cha urais kupitia CCM Dr John Pombe Magufuli akizungumza na wanaccm hao wa mkoa wa Dar es Salaam amesema Tanzania ni nchi ya amani ambayo inapaswa kuendelezwa kwa misingi ya amani bila ukabila na ukanda wala ubaguzi wa aina yeyote na kuwataka watanzania kuendelea kuwa wamoja na kuwahakikishia watanzania kuwa anatosha katika kutatua kero mbalimbali za mtanzania wa kawaida na makundi mbalimbali.
 
Awali, akizungumza na wanaccm mkoa wa Dar es Salaam, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM mikoa Ramadhani Madabida amesema mkutano huo ni wa kwanza tangu kumalizika kwa vikao vya uchujaji wa wagombea katika ngazi zote vilivyoongozwa na mwenyekiti wa chama hicho Dr Jakaya Kikwete na kumhakikishia kuwa wanaccm wa mkoa wa Dar es Salaam wako imara na kwamba wako tayari kwa mapambano ya kisiasa.
 
Katika tukio jingine, mapema asubuhi, Dr John Pombe Magufuli akiambatana na mgombea mwenza mama Samia Hassan Suluhu walirejesha na kusaini fomu za tume ya taifa ya uchaguzi katika mahakama kuu ya Tanzania kwa mujibu wa taratibu na sheria ya tume hiyo ya taifa ya uchaguzi ambapo kwa mujibu wa kanuni na taratibu za tume hiyo wagombea wote wanahitaji kupata wadhamini wasiopungua mia mbili katika baadhi ya mikoa ikiwemo visiwa vya Zanzibar.
 

Post a Comment