gabo
Inafahamika kuwa viongozi wengi wa Afrika wanapenda kujilimbikizia mali na kukaa madarakani ili kuendelea kuongoza nchi zao, wengine husababisha hata nchi kuingia kwenya machafuko ya kisiasa.
Kuna hii ya Rais wa Gabon imenifikia mtu wangu, yeye amewaahidi vijana wa nchi yake kuwapa  urithi wa mali zake.

Ali Bongo Ondimba  amesema mali zote alizopewa na baba yake mzazi Omar Bongo ambaye alitawala Taifa hilo kwa miaka 41 atawapa vijana wa Gabon ikiwemo kuuza majengo mawili ya kifahari yaliyopo Ufaransa.
Kwenye ahadi nyingine ni kwamba jengo moja la kifahari lililoko katika mji mkuu wa Gabon litabadilishwa na kuwa chuo kikuu cha Umma.
Maamuzi ya Rais huyo yamekuja wakati wanasheria wa Ufaransa wakiwa wanachunguza mamilioni ya mali za familia ya Rais huyo zilizotumika kununua na kujenga majumba ya kifahari nchini humo.

Post a Comment