Ikiwa ni siku chache tangu kada wa chama cha mapinduzi CCM Mzee
Kingunge Ngombale Mwiru ajionoe katika chama hicho baadhi ya wazee
wamempongeza.
Miongoni mwa wazee waliojitokeza na kutoa pongezi hizo ni pamoja na
wale wa Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA
ambao wamempongeza kada huyo kwa uamuzi wake.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Katibu
Mkuu wa Baraza la Wazee CHADEMA, Roderick Lutembeka amesema,
wamelazimika kutoa pongezi hizo kutokana na maneno ya Mzee Kingunge kuwa
ya busara na yenye kutaka kulipeleka taifa kwenye maendeleo.
Post a Comment