Chama cha walimu tanzania (CWT)mkoani Kagera kimewaomba  viongozi wa watakao chaguliwa kusimamia serikali ijayo kuhakikisha inalipa deni sugu la malimbikizo ya mishahara ya walimu ambapo mpaka sasa walimu wa mkoa wa Kagera wanazidai halmashauri za wilaya na maspaa  zaidi ya shilingi bilioni tatu.

Hayo yamesemwa katika maadhimisho ya siku ya walimu duniani  na katibu wa chama walimu mkoani Kagera Posian Gelvas amesema walimu wanapata shida katika kudai malimbikizo ya mishahara yao huku serikali ikiwalipa wanasiasa mabilioni ya pesa ambazo zingeweza kusaidia kulipa malimbikizo ya mishahara ya walimu ambayo wanaidai serikali miaka yote na pia zingeweza kuboresha madarasa pamoja na kununua vitendea kazi mashule jambo ambalo wamesema niaibu kubwa kwa serikali  kuona baadhi ya shule zinakosa hata chaki zakufundishia wanafunzi.
 
Mwenyekiti wa chama cha walimu mkoani kagera Dauda Bilikesi akizungumza katika maadhimisho hayo yaliyofanyika kimkoa wilayani Kagara amesema matatizo ya malimbikizo ya mishahara kwa walimu yanasababishwa na baadhi ya waajili  wazembe wanaokiuka sheria  na kutozingatia kanuni na sheria za utumishi wa umama ambapo amebainisha baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikigonga vinchwa vya walimu kila kukichwa kuwa ni mishahara midogo isiyoendana na wakati wa sasa pamoja na walimu wastaafu  kutothaminiwa baada ya utumishi wao kwa muda mrefu.
 
Mkuu wa mkoa wa kagera john mongella ambae alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amesema amelichukua suala hilo nakuwathibitishia walimu kuwa kwaanzia sasa atalisimamia kidete  nakwamba atahakikisha halmashauri zote za wilaya na manispaa za mkoa wa kagera  zinakaa na walimu kwa pamoja ilikuweza kujadili namna ya kuwalipa walimu madai yao.
 
Maadhimisho haya walimu hufanywa na walimu kote duniani ambapo zaidi ya nchi 166 zenye jumla ya vyama vya walimu takribani mianne vikiwa na wanacha milioni therasin na tano ulimwenguni hufanya maadhisho haya  huku chama cha walimu Tanzania (CWT) kikitajwa  kuwa nimiongoni mwa wanachama hai wa shirikisho hilo.

 

 

Post a Comment