![“ Msilinde kura kwa kubaki Vituoni “ – Tume ya Taifa ya Uchaguzi](http://www.timesfm.co.tz/wp-content/uploads/2015/10/1.-Wananchi-wakiwa-kwenye-kituo-cha-kupiga-kura-cha-Kalenga-A-559x520.jpg)
Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini Tanzania – NEC imevitaka vyama vya
siasa kuacha kuwahamasisha wapiga kura kubaki karibu na vituo vya
kupigia kura kwa kigezo cha kulinda kura jambo ambalo ni kinyume cha
sheria, kanuni na maadili ya uchaguzi na sababu za kiusalama.
Tume imetoa wito huo katika mkutano na vyama vya siasa jana jijini
Dar es salaam, uliolenga kuelezea maandalizi ya uchaguzi na namna tume
inavyotumia utaratibu wa kutangaza matokeo ya Udiwani, Ubunge pamoja na
Urais.
Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Mwenyekiti wa tume hiyo
Jaji Mstaafu Damian Lubuva, ametahadharisha kuwa endapo vyama vya siasa
vitaruhusu wapiga kura kubaki vituoni kwa lengo la kulinda kura, upo
uwezekano wa kutokea fujo kwani kwa uzoefu sehemu yenye mikusanyiko ndio
fujo zinapoanzia.
Post a Comment