Akizungumza jana na umati mkubwa
uliofika kushuhudia kampeni za UKAWA katika viwanja vya Tanganyika
Parkers, Kawe jijini Dar es Salaam, Mweneyekiti wa chama cha CHADEMA
Freeman Aikael Mbowe amesema ifikapo oktoba 25 baada ya kupiga kura,
basi ni vyema wakina Mama warudi nyumbani kwa ajili ya kupika na Wanaume
wabaki vituoni ili kulinda kura.
Mbowe amesema oktoba 25 si siku ya
kulala hivyo amewataka wafuasi wa vyama vianavyounda umoja wa katiba ya
wananchi – UKAWA wajitokeze kwa wingi katika kupiga kura na kuhakikisha
hawaibiwi kura zao.
“ Oktoba 25, wakina Mama mkishamaliza
kupiga kura ni bora mkarudi nyumbani kwa ajili ya kupikia awatoto na
wazee, lakini wakina Baba mkimaliza kupiga kura hakikisheni mnahesabu
mita 100 toka kwenye kituo cha kupiga kura na kukaa hapo kwa ajili ya
kulinda kura zenu ”, alisema Mbowe.
Katika mkutano huo vingozi mbali mbali
wa UKAWA wakiongozwa na mgombea wao urais Mh. Edward Lowassa walipanda
jukwaani na kunadi sera zao ambapo wameahidi kuleta mabadiliko endapo
wakipata nafasi ya kuingia madarakani.
Post a Comment