![](http://www.itv.co.tz/media/image/tane07.jpg)
Shirika
la umeme Tanzania -Tanesco limesema hali ni mbaya ya upatikanaji wa
umeme nchini kutokana na chanzo kikuu ambacho ni maji kuzalisha nishati
hiyo asilimia 18 tu ya uwezo wake na kwamba hali hiyo imewafanya
washindwe kuita kukosekana huko umeme nchini kama ni mgawo au dharura.
Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Mhandisi Felchesm Mramba
amesema makali ya tatizo hilo kwa kiasi fulani yamepunguzwa kutokana na
kupatikana kwa nishati ya gesi ambapo pia jumanne ya wiki hii
wamefanikiwa kuwasha megawati 30 kutoka kampuni ya Simbioni.
Post a Comment