Mgombea wa nafasi ya urais kupitia Chadema anayeungwa mkono na vyama vinne vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA Edward Lowassa ameingia mjini Monduli na kupata mapokezi makubwa huku akiahidi kuendelea kushughulikia changamoto za kimaendeleo ndani ya jimbo hilo.
Tofauti na mawazo ya wengi, akiwa monduli kazi yake ya kwanza aliyoifanya ni kumtangaza Bw Julius Kalanga kuwa mrithi wake wa kiti cha ubunge jimbo la Monduli.
 
Mgombea huyo aliyekuwa mbunge wa jimbo la Monduli kwa kipindi cha miaka 20, amewashukuru wakazi wa jimbo hilo kwa ushirikiano waliompatia uliowezesha kupatiakana kwa maendeleo ndani ya jimbo hilo huku akiahidi kuendelea kutekeleza ahadi ambazo bado hajazikamilisha.
 
Edwrad Lowassa ametumia jukwaa la mto wa mbu wilayani Monduli kuwaomba watanzania kuhakikisha wanampigia kura nyingi zaidi kwani uwezo, nia na sababu ya kuwa mshindi wa kiti cha urais anao.
Fredrick Sumaye amewataka wanamonduli na watanzania kwa ujumla kuhakikisha wanaunga mkono kauli mbiu ya mabadiliko kwani umasikini wa watanzania umechochewa na uongozi mbovu wa CCM kwani rasilimali nyingi za nchi zimeshindwa kuwanufaisha watanzania.

 

Katika siku yake ya kwanza ya kampeni kanda ya kaskazini huku akitumia usafiri wa chopa alifanikiwa kuhutubia maeneo ya, Mangora, Mburu na mto wa mbu wilayani Monduli kabla ya kuhutubia maelfa ya wakazi wa mjini Babati mkoani Manyara katika uwanja wa Kwaraa.

Post a Comment