Sakata la Wanafunzi wa Vyou Vikuu na sehemu ya kupiga kura, NEC yashauruiwa.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini NEC imetakiwa iandae utaratibu ambao utawasaidia wananchi wote waliojiandikisha kwenye vituo ambavyo hawawezi kupiga kura waweze kupiga kwani ni haki yao ya msingi.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi Tanzania, Bi Imelda Urio jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Bi Uria amesema kuwa ipo haja kwa NEC kufanya baadhi ya marekebisho katika changamoto kadhaa zilizojitokeza moja wapo ikiwa ni swala la wanafunzi wa vyuo kutokuwa na sehemu ya haki ya kupiga kura ili ifikifika oktoba 25 mapungufu hayo yasiweze kujitokeza na uchaguzi huo ukawa wa huru na haki.
Aidha ameisihi serikali kutofanya mabadiliko tena ya watumishi kwenye Tume hiyo ili kuondoa hali ya wanasiasa kutokuwa na imani na tume hiyo.

 

Post a Comment