Siku chache baada ya kutangazwa kuwa meneja wa klabu ya Liverpool,
Jurgen Klopp ameonyesha nia ya dhati ya kutaka kumsajili kiungo kutoka
nchini Ureno na klabu ya FC Porto, Rúben Diogo da Silva Neves.
Klopp, ameopanga kutimiza dhamira hiyo itakapofika mwezi januari kwa
kuamini usajili wa Nevas utaleta tija kubwa kwenye kikosi chake, ambacho
kitaaza kupata huduma yake mwishoni mwa juma hili wakati wa mchezo wa
ligi kuu ya soka nchini England dhidi ya Tottenham Hotspur.
Nevas, mwenye umri wa miaka 18, amekua katika rada za baadhi ya klabu
kubwa barani Ulaya kama Chelsea, Real Madrid pamoja na FC Barcelona na
inaaminika kama Liverpool wataingia kikamilifu kumuwania, kutakua na
vita kubwa dhidi ya magwiji hao.
Post a Comment