Chama cha NCCR Mageuzi kimemsimamisha kazi Makamu Mwenyekiti wake
Bara Mama Leticia Mosore kutokana na madai kwamba amekiuka Katiba ya
Chama hicho kuwa kumshtumu Mwenyekiti wake Tiafa James Mbatia kwamba
anakihujumu chama.
Hatua ya kumsimamisha imefikiwa septemba 22 mwaka huu, kwa taarifa ya
maneno bila kumpatatia barua kwa lengo la kuendelea kufanya uchunguzi
juu ya malalamiko yaliyotolewa na Mama Mosore.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana,
Mwenyekiti wa NCCR Taifa Mh. James Mbatia ameelezea hatua hiyo
iliyochukuliwa.
James Mbatia amesema Makamu Mwenyekiti huyo alishirikiana na kundi la
wanachama wengine kutunga taarifa za uzushi na kutumiwa na baadhi ya
watu wasiopenda maendeleo ya chama cha NCCR.
Post a Comment