![](http://www.itv.co.tz/media/image/nec07.jpg)
Tume
ya taifa ya uchaguzi imewataka mawakala na jeshi la polisi nchni
kuhakikisha wanatenda haki kwa vyama vyote wakati wa wananchi kupiga
kura ili kuepuka malalamiko yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani
katika vituo vya kupigia kura.
Akizungumza na wasimamizi wa uchaguzi wa nchni nzima na jeshi la
polisi nchni, mnweyekito wa tume ya taifa ya uchaguzi-NEC- jaji mstaafu
Damiani Lubuva amewataka watendaji hao kufuata sheria na kanuni za tume
na kuwataka kutambua kuwa mapungufu madogo yanaweza kusababisha
uvunjifu wa amani.
Kutokana na baadhi ya vyama vya siasa za kuwataka wapiga kura
kubaki katika vituo baada ya kupiga kura jaji Lubuva amewaagiza
wasimamizi wa uchaguzi na jeshi la polisi nchni kutoruhusu watu kusubiri
matokeo ya uchaguzi katika eneo la kupiga kura kwa kisingizia cha
kulinda kura.
Post a Comment