Mradi wa umeme wa gesi asilia ni fursa ya maendeleo kwa watanzania – Rais Kikwete.

Rais Jakaya Kikwete jana amezindua rasmi kituo cha kufua umeme kilichopo kinyerezi jijni Dar es Salaam hatua ambayo inaashiria mgao wa umeme nchini kuanza kupungua siku hadi siku.

Akizindua kituo hicho, Rais Kikwete amesema kuwa uamuzi huo unaenda sambamba na mpango mpya ambao unatarajia kuanza mwakani utakaoibua fursa za uchumi wa maendeleo kwa watanzania baada ya kunufaika kwa kuwa na umeme wa uhakika.

Aidha Rais Kikwete amebainisha kuwa hadi sasa vyanzo vyote vilivyopo vya umeme wa maji havijaweza kufikisha kiasi kinachotakiwa kusambaza umeme nchi nzima hivyo kwa hatua hiyo ya kuanza kutumia umeme wa gesi kutarahisisha ugawaji wa umeme sehemu mbalimbali nchini.

Hata hivyo Rais Kikwete ameendelea kusema kuwa katika mipango ya maendeleo inayotekelezwa hivi sasa ya miaka mitano ambayo inaisha mwaka ujao lengo lilikuwa ni kufikisha umeme wa megawatts 2780 ambapo amesema kuwa bado jitihada zinafanyika ili mwaka ujao wafikie malengo hayo.

Post a Comment