![](http://www.itv.co.tz/media/image/mgomo%20moro.jpg)
Madereva
wa daladala mkoani Morogoro wamegoma kutoa huduma za usafirishaji
wakishinikiza kutatuliwa kwa changamoto mbalimbali zinazowakabili
sambamba na kuachiwa kwa wenzao wawili waliokamatwa siku takribani sita
zilizopita kwa madai ya kutishia kumgonga askari wa usalama barabarani
na mwingine kudaiwa kusafirisha mafuta ya petroli kinyume na utaratibu.
Wakizungumza na ITV baadhi ya madereva wameeleza kusikitishwa na
uonevu waliodai wenzao kufanyiwa na baadhi ya viongozi wa jeshi la
polisi kwa kubambikiwa makosa huku wakinyimwa dhamana au kufikishwa
mahakamani, kukamatwa na maafisa wa mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa
majini na nchi kavu Sumatra kwa madai ya kuibia njia pale wanapoamua
kusaidia huduma maeneo ya mbali ambayo hayajapangiwa njia rasmi na ubovu
wa muda mrefu wa miundo mbinu.
Kufuatia mgomo huo, adha kubwa imewakumba wananchi wakiwemo
wanafunzi na wakazi wengine, huku wengi wakishindwa kwenda makazini na
kwenye shughuli zao hvyo kulalamikia mamlaka husika kushindwa kutatua
changamoto hizo hadi kusababisha mgomo huo.
Akizungumza baada ya kikao cha dharura kilichoshirikisha uwakilishi
wa madereva, jeshi la polisi, Sumatra na viongozi wa manispaa, kamanda
wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amesema wamekubaliana madereva
hao kusitisha mgomo na kurudi barabarani, na kwamba wataimarisha
ushirikiano miongoni mwao na kwa pamoja kutatua kero zilizolalamikiwa.
Post a Comment