Jokate:wasanii waache kuvimba vichwa.

Wasanii nchini wamekumushwa kuwa njia pekee ambayo itawawezesha kuwa na mafanikio katika fani zao ni kufanya kazi kwa heshima bila kubaguana huku wakitambua kuwa hawawezi kuwa ‘matawi ya juu’ siku zote.

Hayo yamesemwa na mwanamitindo na muimbaji,Jokate Mwegelo,ambaye amewataka wasanii kutumia umaarufu wao vizuri ili wapewe ushirikiano na kila mtu katika kazi zao.

”Nimesema hivyo kwa sababu baadhi ya wasanii wanavimba kichwa baada ya kupata umaarufu hali ambayo mwisho wao huwa ni mbaya kwenye kazi zao,”

”Msanii akiwa maarufu kila mtu akawa anaimba nyimbo zake ni rahisi kuvimba kichwa na kujiona yeye ndio yeye,anasahau kabla ya yeye kulikuwa kuna watu ambao walikuwa juu yake,”alisema Jokate.
Jokate alisema kuwa njia pekee ambayo itawasaidia wasanii na hasa wa muziki wa kizazi kipya ni kutambua umuhimu wao kwenye fani hiyo pamoja na nafasi ya wasanii wenzao na kuacha kujiona ni bora kuliko wengine.

Post a Comment