SeeBait
Agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mkoani Geita la kuwagawia wananchi mabaki ya mawe maarufu kama Magwangala kutoka mgodi wa dhahabu wa Geita GGM umeanza kutekelezwa.

Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Sospeter Muhongo yupo katika ziara ya kikazi katika mgodi huo kwa kutafuta sehemu ambayo wachimbaji watayaweka na kuyachenjua kwa ajili ya kuyagawa kwa wananchi.

Akiongea mara baada ya ziara hiyo Mhe. Muhongo amesema kuwa agizo la Rais lilikuwa ni baada ya wiki tatu lakini kwa kuwajali wananchi wa eneo hilo wameamua kuanza zoezi hilo mapema kwa ajili ya utekelezaji wa agizo la rais.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Emanuel Kiunga, amesema kuwa serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na wabunge wa mkoa huo na baadhi ya viongozi wametafuta maeneo ya kuweka Magwangala hayo kwa ajili ya kuyahifadhi.

Wakizungumzia maeneo hayo yaliyotengwa kwa ajili ya zoezi hilo baadhi ya wabunge wa mkoa huo akiwemo Mbunge wa viti Maalum kwa tiketi ya CHADEMA, Upendo Peneza, na Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku Musukuma wamesema serikali lazima iwe makini na mawe hayo pamoja na kuwajali wananchi wa maeneo yaliyotengwa.

Post a Comment

  1. What are the differences between casinos and online gambling?
    Here 청주 출장마사지 you will find 여주 출장안마 all information 제천 출장안마 about different types of 전라북도 출장샵 online gambling. We will present you all information about the games you can play 수원 출장샵 and how many

    ReplyDelete