Njia mpya ya kutia
dawa za kuua mbu kwenye vyandarua imefanikiwa kwa asilimia 100 katika
kukabili baadhi ya aina za mbu, ripoti ya utafiti wa kimataifa inasema.
Njia hiyo inayotumia nguvu za umeme za elektrostatiki kupaka dawa huwezesha vyandarua kubeba viwango vya juu vya dawa.
Mbu kuzoea dawa limekuwa tatizo sugu katika maeneo mengi yanayotatizwa na malaria duniani.
Inadhaniwa
dawa za maji za kunyunyizwa pamoja na neti za vitanda, ambazo mara
nyingi huwa na viwango vya chini vya dawa, huwa mara nyingi haziui mbu,
na kuwafanya kuzoea dawa.
Kwenye utafiti wa sasa, watafiti kutoka Uholanzi, walitumia sehemu
yenye nguvu za umeme, iliyotayarishwa awali kwa kunasa chavua hewani, na
kuipaka dawa.
Kutumiwa kwa nguvu za umeme aina ya electrostatic
zinazodumu muda mrefu kuliwezesha viwango vya juu vya dawa kujishikilia
upesi na vyema kwenye vyandarua, na kuhakikisha mbu wanapata dawa ya
kutosha kuwaua wanapogusa neti - hata kama ni sekunde chache tu.
Mbinu
hiyo ilifanyiwa majaribio kwenye aina tofauti tofauti za mbu Afrika
Kusini, Tanzania na kwenye maabara ya kitivo cha dawa za maeneo yenye
mvua nyingi cha Liverpool.
Watafiti walibaini kuweka dawa kwa
kutumia nguvu hizo za umeme kuliwezesha kuuawa kwa mbu wengi,
ikilinganishwa na neti zilizopakwa dawa kwa njia nyingine na kwa baadhi
ya mbu ambao wamekuwa hawasikii dawa, ilifanikiwa asilimia 100.
aliyeongoza
utafiti huo, kutoka In2Care, katika Chuo Kikuu cha Wageningen, nchini
Uholanzi, amesema njia hiyo ya kupaka dawa inaweza kutumiwa kwenye
vitambaa vya kufunika madirisha na milango nyumbani, na kwenye mitego ya
mbu na mashimo ya kupitishia hewa manyumbani.
"Ni njia mpya ya kulenga kuwafikia na kuwapa dawa mbu," amesema.
Aidha, amesema njia hiyo mpya itafaa sana kwani inaweza kutumiwa na aina mbalimbali za dawa.
Hata
hivyo, amesema njia hiyo ya kupaka dawa huenda haifai kwa neti za
kufunika vitanda kwani watu huzigusa mara kwa mara na kwa hivyo dawa
hiyo inaweza kutoka baada ya muda.
Post a Comment